![]() |
Mkandarasi Geofrey Mungai akimnywesha uji mtoto wa kituo cha yatima Tosamaganga jana baada ya kufikia kituoni hapo kutoa msaada wa chakula cha sikukuu |
![]() |
Mungai akitoa msaada wa mafuta na vyakula kituo cha watoto yatima Tosamaganga |
Mtoto yatima wa kituo cha Tosamaganga akifurahi na Mungai
![]() |
Mungai akiwa na watoto yatima wa kituo cha DBL |
MKANDARASI maarufu mkoani Iringa Geofrey Mungai ametoa msaada wa chakula cha Mwaka mpya chenye thamani ya shilingi milioni 3 kwa vituo vitatu vya yatima kikiwemo cha Daily Bread life childreans home (DBL)cha mkimbizi katika Manispaa ya Iringa huku akimpongeza Rais Dkt John Magufuli kwa kuendelea kusaidia yatima Iringa.
Akikabidhi msaada huo jana kwa nyakati tofauti katika kituo cha DBL ,Lugalo na Tosamaganga ,Mungai alisema kuwa umekuwa ni utamaduni wake na familia yake kutoa chakula na mavazi kwa yatima siku za sikukuu kila mwaka
Mungai alisema kuwa amelazimika kutoa zawadi hizo za sikukuu kwa watoto hao kama njia ya kuwajali na kuwafanya yatima hao kufurahia sikukuu kama watoto wenye wazazi .
Hata hivyo alitaka jamii kuendelea kuwakumbuka watoto hao yatima badala ya kuendelea kuwatenga na kuwanyanyapaa kwa madai kuwa watoto hao yatima hawakupenda kuwa yatima ila ni mipango ya Mungu na kuwa jamii kuendelea kuwabagua ni kuongeza unyanyapaa kwa watoto hao wasio na hatia mbele za Mungu.
Pia alisema kuwa kupitia kampuni yake ya ukandarasi mkoani Iringa amekuwa na kawaida ya kutenga bajeti kwa ajili ya kuwasaidia watoto wa kituo hicho cha DBL na vingine mkoani Iringa na kuwa ataendelea kufanya hivyo kwa kuwaweka jirani zaidi watoto hayo kama sehemu ya familia yake.
Aidha Mungai alipongeza jitihada kubwa zinazofanywa na uongozi wa kituo hicho katika kuwalea yatima hao na kuwa mbali ya kuwepo kwa vituo vingi vya yatima ila kituo hicho kimekuwa kikiwalea yatima hao kama familia na kuwa ni vigumu kuweza kuamini kama watoto hao ni yatima kutokana na maisha wanayoishi kituoni hapo.
Alisema jitihada mbali mbali zimekuwa zikifanywa na vionngozi wa serikali akiwemo Rais Dkt Magufuli kuona jamii yenye matatizo wakiwemo yatima hao wanapata zawadi mbali mbali kipindi cha sikukuu.
Hivyo aliiomba jamii kuiga mafano wa Rais katika kuwajali watoto yatima kwa kuwakumbuka wakati wa sikukuu mbali mbali .
mkurugenzi mtendaji wa kituo hicho mchungaji Mpeli Mwaisumbe mbali ya kumpongeza Geofrey Mungai na familia yake kwa kutoa msaada huo pia alisema kuwa Mungai amekuwa bega kwa bega na kituo hicho .
Mchungaji Mwaisumbe aliwataka viongozi wa dini kufanya kai ya kuliombea Taifa pamoja na Rais Dkt Magufuli kwa kazi kubwa na nzuri anayoifanya badala ya viongozi wa dini kutumia nyumba za ibada kuishambulia serikali .
Mkurugenzi wa kituo hicho Mchungaji Neema Mpeli akishukuru kwa msaada huo alisema kuwa jitihada zinazofanywa na mkandarasi Mungi katika kuwakumbuka watoto hao ni kubwa na kuwa amekuwa kiunganishi kati ya watoto hao na familia yake .