
KAMPENI ya kupambana na fistula hapa nchini ilizinduliwa Oktoba 16 mwaka 2010,ambapo kwa wakati huo kulikuwa na kuna kesi mpya wa 3000.
Unganga na mwandishi wa mtandao huu kutoka Wilaya ya Njombe Marcy James anaelezea Katika makala haya anasema kuwa kipindi hicho hapa nchini ilibainika kuwa ni
wanawake 800 kwa mwaka wanaoweza kupata msaada na
upasuaji ambapo mara nyingi sana hubaki na lemavu.
Takwimu hizi ni taarifa katika mwanzo wa kampeni ya
elimu kwa wanawake taarifa, ambayo mara nyingi husababisha kutengwa na familia zao na jamii,ili
hali inaweza kutibiwa.
Ugumu wa kupatiwa matibabu unatokana na gharama ya
upasuaji kutibu hali, na gharama ya malazi wakati a
kusubiri matibabu, ambayo inaweza kuchukua hadi wiki sita, na pia gharama ya kupata hospitali ambayo
inaweza kufanya upasuaji.
Maendeleo ya haraka yamepatikana katika miaka ya hivi karibuni, ambapo kwa kazi ya Pioneering Reginald na Catherine Hamlin wa nchini Addis Ababa kuanzia mwaka 1960.
Hata hivyo mafunzo bado ghali na hii, pamoja na wamba operesheni inachukua muda kutoka upasuaji na tiba mwisho, kwa kawaida hufanya gharama za matibabu nje ya uwezo wa wanawake ambao wanateseka zaidi kutokana na hali hiyo.
Katika maeneo ya vijijini matatizo hayo huwakumba
akina mama ambao hukosa msaada muda wa kujifungua
unapowadia, hali hiyo mara nyingi inatokana na maisha duni,umasikini uliopo kwa watanzania walio wengi.
Hali hiyo imekuwa ikisababisha wanawake kuzaa kwa
taabu chini ya uangalizi wa wakunga wa jadi ambao si wataalamu wa mtatizo ya uzazi hususani pale inapobainika mama mjazito anaye mhudumia anatatizo la kyutofunguka njia ya uzazi ambapo kitaalamu angehitaji upasuaji.
Utafiti unaonesha kila siku wanawake wasiopungua 273 wamekuwa wakipata ugonjwa huu na kuumia wakati wa kujifungua.
Idadi ya wanawake wenye matatizo ya Fistula inazidi
kuongezeka zaidi Kila mwaka takriban 100,000 wanawake kuendelea kupata matatizo hayo na uwezo wa mataifa wa kutibu wagonjwa hupo imekadiriwa katika mwaka wagonjwa 6500 au wagonjwa 18 kila siku.
Kati ya wagonjwa hao, walio wengi wamekuwa wakishindwa kutambua wapi wataweza kumaliziwa tatizo lao kwa mtazamo huo dume wanaishia kubaki na ugonjwa huku wakitengwa na wanandoa wao kutokana na kero ya ugonjwa huo bila huruma huwatenga pengine huwafukuza katika nyumba zao.
Hayo yote sababu kubwa ni akina mama wengi katika
nchi maskini kujifungua bila msaada wowote wa
matibabu,ikiwepo na wasichana wanaojifungua wakiwa
katika umri mdogo.
Mwandishi wa makala hii katika pita pita yake
anakutana na mama ambaye alijitambulisha kwa jina la Bi.Elizabeth Rajab (37)mkazi wa kijiji cha cha Mlowa Wilaya ya Njombe Mkoa wa Iringa.
Bi. Elizabeth yeye kwa upande wake anaelezea jinsi
ambavyo alipata ugonjwa wa Fistula uliosababisha
kuvunjika kwa ndoa yake hadi sasa ametengana na mume wake.
Anasema,amebahatika kuzaa watoto sita pasipo kupata
matatizo lakini alipopata ujauzito wa saba alikutana
na matatizo ambayo anasema, kwake ulikuwa msalaba wake peke yake.
Anasema, mwaka 2007 ujauzito wake ulipotimiza miezi
tisa alipata uchungu wa kujifungua, kwa kuwa alikuwa
kijijini alikosa msaada kwa ndugu zake ambao walidhani uzazi unafanana bila kujali hawakuchukua hatua yoyote wakidhani atajifungua salama chini ya wakunga wa jadi kama ilivyozoeleka.
Ilikuwa Februali 15 alipopata uchungu wa kuzaa, na
mtoto alianza kutoka kwa kutanguliza mkono katika njia ya uzazi ambapo alikaa na mtoto katika mlango wa uzazi hadi siku ya pili februali 16.
Hali ya mama huyo ilikuwa hivyo mtoto akiwa mlangoni
kwa siku mbili ambapo alipofikishwa hospitali ya Wilaya Kibena Njombe alikosa msaada wa daktali kwa maelezo kuwa upasuaji ungefanyika kesho yake siku ya tatu.
Anasema alikaa katika hali hiyo hadi asubuhi ambapo
alifanyiwa upasuaji na kutoa mtoto ambaye hakua hai kutokana na uchungu wa mda mrefu ambao amekaa nao.
Mama huyo anasema,alipofanyiwa upasuaji na kutoa
kiumbe mfu aliendelea kupata maumivu na kutokwa maji sehemu zake za siri ambapo aliambiwa na wauguzi kuwa ni hali ya kawaida ni kutokana na mipira uliowekewa kutolea haja ndogo baada ya kufanyiwa upasuaji.
Anasema, licha ya kuwa katika hali hiyo alizidi kupata maumivu makali ya tumbo, wakati huo hakuwa na ndugu na hata mumewe pia alimwacha hapo hospitali bila msaada ambapo alikula kwa kutegemea msaada wa wagonjwa na kwamba kuna wakati alikunywa maji yaliyopo vyooni kwa kukosa huduma za ndugu zake.
Anasema alika hapo hadi siku ya saba ambapo mumewe
alipata taarifa juu ya yaliyotokea na kuomba kibali
cha kuondoka nae hadi nyumbani, ambako hali yake ilizidi kuwa mbaya.
Akisimulia kwa uchungu anasema, alipelekwa Hospitali
ya Peramiho kwa matibabu zaidi ambapo yake hali
haikubadilika kwani alikuwa akitokwa haja kubwa na
ndogo pasipo taarifa, kwa hali hiyo alipata kipigo kutoka kwa mumewe kila alipotoka kwenye pombe kwa madai kuwa anamkera.
Akiwa hospitalini Peramiho alipewa masharti ya
kutojihusisha na tendo la ndoa hadi atakapopata
matibabu, anasema, kwa wakati huo mumewe alikubali
alipofika nyumbani hali ilikuwa tofauti na
alivyotegemea.
Anasema, alikuwa katika mateso makubwa, mume alikuwa akimfanyia vitendo vya unyanyasaji kama kunyimwa huduma muhimu kama mgonjwa,kubakwa kila aliporejea usiku kutoka kulewa,na kisha kufukuzwa katika chumba na kulala
mahali
ambapo si salama kiafya kwa madai kuwa hatakiwi kulala karibu na mumewe.
Kwa kipindi hicho alipokuwa akijaribu kumshauri mumewe
kuacha tabia ya kumbaka kila siku na kumweleza jinsi
anavyojisikia haikumsaidia, kutokana na hali yake
kiafya alipata kichapo na kupewa lugha za matusi yenye kudharirisha.
Hali hiyo ilimsababishia kuondoka nyumbani kwani
hakuna na msaada ndipo alipopata msaada kwa wasamalia wema ambao walimpa hifadhi wakati akisubiri msaada wa matibabu baada ya kusikia kuna tiba ya Fistula.
Katika kipindi cha miaka mitatu aliishi maisha ya
kutengwa na jamii, ndugu wa mumewe na hata majirani waliona kuwepo karibu naye ni kero kwa sababu ya
harufu aliyokuwa nayo.
Anasema, mwaka 2010 alipata msaada wa kupelekwa tasisi ya CCBRT jijini Dar es Salaamu ambapo alipatiwa matibabu na kupona msiba wake hali iliyosababisha ndugu kurejea na kumtaka radhi arudiane na mumewe kitu ambacho anasema
hawezi kukikubali.
Anasema, kupitia tatizo hilo aliweza kumtambua nani
rafiki na adui yake ni nani, hata hivyo anatoa ushauri kwa wanawake wenye matatizo kama yake wasijifiche wajitokeze ili kupata matibabu ambayo yanatolewa bila gharama yoyote.
Bw.Shaban Pella mkurugenzi wa taasisi isiyokuwa ya
kiserikali inajihusisha na masuala ya watoto waishio
katika mazingira hatarishi ya mjini Makambako
anasema, katika uchunguzi wake ambao amefanya amegundua wapo akina mama wanaoishi na tatizo hilo bila matibabu.
Pella anasema,alipogundua tatizo hilo lipo katika
Wilaya ya Njombe alifanikiwa kutoa msaada wa kuwasafirisha wanawake 13 ambao wamepata matibabu CCBRT na kwamba wamepona akiwemo Bi.Elizabeth.
Anasema, ingawa wapo wanawake ambao wanajificha maeneo ya vijijini ambao ni wengi na wanakabiliwa na matatizo ya Fistula kwa miaka mingi hata zaidi ya hao ambao amepatiwa matibabu.
"Tatizo lililopo katika wilaya yetu ni mila potofu,
watu wanaamini kuwa ni aibu kujitangaza ugonjwa walio nao wakidhani kwamba ipo siku watapona kwa miti shamba".
"Wapo ambao wanateseka kwa kipindi kirefu sasa, ingawa mchakato wa kuwasaidia kwa mara nyingine upo
unaendelea, lakini wanawake wapo na wanateseka sana na Fistula" anasema BW.Pella.
Anasema, wanawake ambao wamepata matibabu katika
kipindi cha mwaka mmoja tangu alipofanya jitihada hizo nikutoka katika vijiji vya kifumbe,Katenge,Ikwete na Ikulimambo.
Mwisho.